Sunday 28 April 2013

Akisoma hotuba ya kambi hiyo kuhusu makadirio ya bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Msemaji Mkuu wa mambo yanayohusu wizara hiyo, Rose Kamili alisema wanahitaji maelezo kwa sababu ni miaka michache imebaki kukamilika kwa utekelezaji huo




Mtoto akipalilia shamba la mpunga wilayani bariadi mkoa wa Simiyu hivi karibuni, mvua zinazoendelea kunyesha zinaleta matumaini ya kupatikana kwa chakula nchini katika msimu huu. Picha na Mpoki Bukuku


Kambi ya Upinzani Bungeni,imeitaka Serikali kueleza kwa kina utekelezaji wa nguzo kumi za Kilimo Kwanza, kwa kuzingatia kuwa imebaki miaka miwili kukamilika utekelezaji wa dhana hiyo.
Akisoma hotuba ya kambi hiyo kuhusu makadirio ya bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Msemaji Mkuu wa mambo yanayohusu wizara hiyo, Rose Kamili alisema wanahitaji maelezo kwa sababu ni miaka michache imebaki kukamilika kwa utekelezaji huo.
Kamili alitaja nguzo hizo kuwa ni dira ya kilimo kwanza, kugharimia kilimo, muundo mpya wa taasisi ya usimamizi, mabadiliko ya mfumo wa mkakati na ardhi kwa ajili ya kilimo.
Nyingine ni sayansi, teknolojia na rasilimali watu, miundombinu kwa ajili ya kilimo kwanza na uhamasishaji wa Watanzania kuhusu kilimo. Kamili alisema kambi ya upinzani inataka majibu ya kina kama Sh60 bilioni zilizotolewa badala ya Sh750 bilioni zilizopangwa kwa ajili ya uanzishaji wa Benki ya Kilimo, zitatosha kulingana na mpango wa utekelezaji.
“Pia, tunataka kujua kama mtaji huu wa Sh60 bilioni ni sehemu ya marejesho ya fedha za EPA kama Bunge lilivyokuwa limeelezwa kuwa fedha za EPA zitaelekezwa kwenye kilimo,” alisema Kamili.
Mbunge huyo alisema mwenendo wa kilimo nchini tangu mwaka 1996 kwenye uchumi wa nchi, umekuwa ukikua kati ya asilimia 3.5 na 7.8 kwa mwaka na kwamba hiyo inaonyesha kuwa kasi ya ukuaji inapungua

Wednesday 24 April 2013

Wizara Kushirikiana na Indonesia Kukuza Kilimo



Naibu Katibu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bi. Sophia Kaduma wa nne Kulia, akiwa  pamoja na Tume ya Ushirikiano wa Pamoja katika sekta ya kilimo.

Tume ya pamoja ya Ushirikiano katika sekta ya kilimo  ya Wizara ya Kilimo Chakula na ushirika imejadili maeneo ya kushirikina kwa awamu ya pili na serikali ya Indonesia  ili kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo.
Akizungumza na tume kutoka pande zote mbili Tanzania na Indonesia Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mama Sophia Kaduma alisema majadiliano hayo yanalenga kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo pamoja na upatikanaji wa masoko.
Mama Kaduma alisema ushirikiano baina ya nchi hizo mbili utahusisha katika kujenga uwezo wa wakulima, masuala ya utafiti pamoja na upatikanaji wa masoko ya mazao.
Katika kujenga uwezo Mama kaduma alisema Tanzania na Indonesia itashirikiana katika mafunzo ya Muda mfupi na mrefu pamoja na kubadilishana wakufunzi ambao wataenda kufundisha vyuo mbalimbali vilivyopo katika nchi hizo.
Katika mafunzo ya muda mfupi serikali ya Indonesia itafadhili  masomo ya  Uchumi Kilimo na kilimo cha bustani hasa katika maeneo  ya utafiti, usindikaji na mbegu.

Alifafanua kukuwa Indosesi itafadhili mafunzo kwa wakulima 15 chini ya mpango wa Ushirikiano wa nchi za kusini   ambapo wakulima 12 watatoka Tanzania Bara na watatu watatoka Tanzania Visiwani.
Aliongeza kuwa masoma hayo yataanza tarehe 1-9/07/1213 na Tanzania itagharamia nauli za washiriki wa program hiyo pamoja na pesa za kujikimu.
Kwa upande wa mafunzo ya muda mrefu katika kujenga uwezo, serikali ya Indonesia itatoa ufadhili kwa watu watatu  ambao watasoma shahada ya uzamili na uzamifu na mmoja  ambaye atasoma masomo  yalio chini ya shahada ya kwanza.
Pia alisema nchi hizo mbili zitashirikana katika mambo ya utafiti wa mazao hasa katika mazao ya pamba, mpunga na viungo mbalimbali.
Alifafanua kuwa utafiti huo utahusisha mambo ya GMO, majaribioa mashambani, uzalishaji wa mbegu bora, magonjwa, usindikaji na uimarishaji wa vituo vya utafiti.
Mama Kaduma alisema pian nchi hizo zimekubalia kushirikiana katika katika masoko kwa kubadilishana taarifa za masoko na taratibu mbalimblia ili kuboresha biashara ya bidhaa za kilimo kati ya nchi zote mbili.
Alifafaunua kuwa licha ya kushirikiana katika masoko pia Serikali ya Indonesia itashiriki katika maonesho ya kimataifa ya wafanya biashara yafanyika Dar es Salaam (Sabasaba) pamoja na maonesho ya wakulima ya Nane Nane.
Ushirikianao baina ya nchi hizo mbili unalenga kuongeza tija katika kilimo, kuongeza upatikanaji wa masoko, kuongeza uzalishaji wa mazao pamoja na kukuza kipato cha mkulima.