Monday 13 May 2013

FANYA MAHARAGE IWE MKOMBOZI


MBEGU BORA ZA MAHARAGE

Aina mbili ya mbegu bora za maharage zimeendelezwa/zimezalishwa katika kituo cha utafiti wa kilimo kilichopo Uyole mkoani mbeya. Mbegu hizo ni BILFA 16 na UYOLE 04. Kuzalishwa kwa mbegu hizi bora ni juhudi za muda mrefu za mpango wa kuzalisha mbegu bora za maharage lengo likiwa ni kuongeza uzalishaji na maharage yakiwa katika sifa na ubora unapendekezwa na wakulima pamoja na walaji, wakulima hupendelea mbegu zinazohimili magonjwa, zinazohimili ukame na zenye mazao mengi wakati walaji hupendelea maharage yenye ladha nzuri na yanayoiva kwa urahisi yakiwa katika bei yenye unafuu.

Mbegu ya UYOLE 04 hutambaa, huzaa maharage yenye ukubwa wa wastani mpaka kubwa kabisa zikiwa na rangi ya maziwa, zinahimili magonjwa sugu kama kutu ya maharage na anthracnose, huiva haraka yakipikwa na huwa na ladha nzuri sana

Wakati wa kupanda mbegu hii hutegemea msimu wa kuanza na kuisha kwa mvua, kwa mfano sehemu ambazo mvua huisha mwisho wa mwezi wa 4 au mwanzo wa mwezi wa 5 basi upandaji uanze mwezi wa 3 kwa sababu ukuaji wa mbegu hizi mpaka kukomaa huchukua wastani wa siku 105. Kiasi cha mbegu zinazohitajika kupanda ni kilo 70 – 80kwa hekta ambapo miche 200,000 huota na huweza kuzalisha kiasi cha tani 1.5 – 1.8kwa kila hecta, mbegu hii hufaa sana kupandwa nyanda za juu kaskazini (mikoa ya Mbeya, Iringa, Songea na Rukwa) ambako ardhi imeinuka wastani wa mita 800 – 2000kutoka usawa wa bahari na kuna baridi.


BILFA 16

Mbegu ya BILFA 16 huwa na rangi nyekundu mchanganyiko na maziwa kama nguo ya jeshi, mbegu ni za ukubwa wa wastani, huweza kuhimili sana magonjwa, mimea ni ya kijani kibichi yenye majani madogo madogo huwa na matawi 4 – 5 maua huwa na rangi ya pinki na vishubaka vya maharage huwa vyeupe na vikikomaa huwa rangi ya maziwa

. Kiasi cha mbegu zinazohitajika kupanda ni kilo 70 – 80 kwa hekta ambapo miche200,000 huota na huweza kuzalisha kiasi cha tani 1.2 – 1.5 kwa kila hecta, ambacho ni kidogo ukilinganisha na UYOLE 04, mbegu hii hufaa sana kupandwa nyanda za juu kaskazini (mikoa ya Mbeya, Iringa, Songea na Rukwa) ambako ardhi imeinuka wastani wa mita 800 – 2000 kutoka usawa wa bahari na kuna baridi. Na mbegu hii hukoma baada ya siku 80 – 84 tangu kupandwa kwa hiyo hufaa kwenye maeneo yenye mvua za muda mfupi

Friday 10 May 2013

Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai



Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo.

Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja hutengeneza rutuba kwenye udongo.

Utunzaji wa rutuba ya udongo unaongozwa na filosofia hii ‘Lisha udongo ili nao ulishe mimea.’ Udongo wenye rutuba utazalisha mimea yenye afya inayoweza kukabiliana na magonjwa. Uzalishaji wa mazao kwa njia za asili uhakikisha kunakuwepo uzalishaji wa kutosha bila ya kutumia pembejeo za ziada isipokuwa matandazo, mboji na bila kutifua udongo mara kwa mara. Ongezeko la malighafi za asili husaidia kuimarisha udongo na kufanya kuwepo kwa virutubisho vya kutosha.

Athari kwa afya ya mimea

Kwa bahati mbaya, aina ya kilimo cha kisasa na kinachotumia kemikali hufanywa tofauti na ilivyo kwa kilimo hai. Katika aina hii ya kilimo; udongo hulimwa mara kwa mara jambo linalosababisha uharibifu wa muundo wa udongo, uwiano wa virutubisho, ambapo virutubisho huongezwa kwa kutumia mbolea za viwandani na matandazo hayazingatiwi. Muundo wa udongo unapobadilika, rutuba nayo hupungua, uwezo wa udongo kwenye udongo pia hupungua.

Kiwango cha udongo mzuri pia hupungua kwa kuwa hakuna tena viumbe hai wanaotengeneza udongo ila unapungua kila msimu wa mavuno. Kwa asili mzunguko huu huwa na matokeo yanayoishia kwenye afya ya mimea, na hapa wadudu huchukua nafasi inayowawezesha kufikia malengo yao.

Ziba pengo

Wakulima wanatakiwa kuhakikisha kuwa kuna virutubisho vya kutosha shambani mwao kila wakati. Ikiwa kuna mwanya pale ambapo baadhi ya pembejeo zinakosekana, kununua virutubisho kwa ajili ya udongo vilivyomo kwenye mfumo wa mbolea za asili inaruhusiwa. Hata hivyo, weka utaratibu wa kuwa na virutubisho kutoka shambani mwako muda wote.

Endapo tukitegemea kulisha udongo kutokana na mbolea za viwandani na kutumia virutubisho vya asili, bado tutakuwa tunafanya sawa na yanayofanyika katika kilimo cha kisasa. Tutakuwa hatujauongezea udongo uwezo wa kujitengeneza na kuongezeka, jambo ambalo ndio msingi muhimu wa kilimo hai.

Vyanzo vya virutubisho

Mimea inayofunika udongo – Mimea inayotambaa huongeza na kushika virutubisho kwenye udongo, kuongeza malighafi zinazooza kwenye udongo, kuzuia madini ya naitraiti kuzama kwenye udongo, virutubisho kutiririshwa, na mmomonyoko wa udongo. Jambo la muhimu hapa ni kuwa udongo umefunikwa ili kuzuia uharibifu. Mimea jamii ya mikunde inapendekezwa zaidi kwa kuwa
husaidia kuongeza nitrojeni kwenye udongo inayopatikana hewani.

Inashauriwa pia kuchanganya mimea jamii ya mikunde na nyasi kwa kuwa nyasi hutumia nitrojeni nyingi sana kutoka kwenye udongo, hivyo itasaidia kutokuharibika kwa mtiririko mzima wa uwekaji wa nitrojeni kwenye udongo.

Mboji - Mboji hasa inayotengenezwa kwa kutumia kinyesi cha wanyama, inaweza kuwa chanzo kizuri cha viumbe wadogo kwenye udongo na virutubisho vyenye gharama ndogo. Unapotumia mboji, changamoto kubwa ni kuhakikisha kuwa imeoza vizuri na namna ya kuitumia kwa usahihi. Endapo mchanganyiko uliotumika kutengeneza mboji hiyo yalikuwa na ubora wa chini, basi mboji hiyo nayo itakuwa na ubora mdogo sana. Itakuwa vizuri kama wakulima hawataacha mboji ikapigwa na jua au mvua, kwa kuwa hali hii inaweza kusababisha kupotea kwa virutubisho kwenye mboji. Kinyesi cha mifugo huboresha mboji zaidi.

Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kuwa kiasi cha 15% ya virutubisho vinavyopatikana kwenye mboji hutumika shambani kwa mwaka wa kwanza. Hivyo, matumizi ya mara kwa mara ya mboji yanapendekezwa ili kuweza kuongeza nitrojeni na malighafi zinazo oza kwenye udongo.

Samadi - Samadi inayotokana na wanyama waliokomaa inaweza kuwa na uwiano mzuri wa virutubisho vya nitrojeni na aina nyingine kwa kiasi kidogo. Tatizo moja la samadi ni upatikanaji pamoja na kutokuwa na ubora unaofanana wakati wote. Kiasi kikubwa cha samadi inayotumika kwenye shamba la mboga, huozeshwa kabla ya kutumika, jambo linalosaidia kupunguza madhara kwenye vyakula.

Malengo kwa ajili ya udongo na mazao
•  Kuongeza malighafi zinazo oza kwenye udongo
• Kuboresha muundo wa udongo
• Kuwezesha upatikanaji wa nitrojeni
• Kuongeza uwezo wa uhifadhi wa rutuba
• Kujenga uwepo wa uhai wa viumbe hai kwenye udongo
• Kufifisha magonjwa ya mazao
• Kujenga mazingira ya udongo wenye uwiano

Kilimo hai ni mkombozi wa mkulima Tanzania

Kilimo ndio msingi wa maisha ya binadamu, na kwa Mtanzania, tunaambiwa daima kwamba kilimo ndio uti wa mgongo wa uchumi, kikiwa kinachangia asilimia kubwa ya pato la taifa, na pia kilimo ndiye mwajiri wa takriban asilimia 80 ya Watanzania.
Kama viongozi wetu walivyopata kutueleza, ili tuweze kupata maendeleo, ni lazima kuwepo na vitu vitatu: Ardhi, Uongozi Bora na Siasa Safi. Tayari vitu hivi vipo kwa sababu taifa letu linaendeshwa kwa misingi ya demokrasia, na ardhi ipo ya kutosha.
Hata hivyo, ni lazima kutambua kwamba, ardhi ama udongo ndiyo rasilimali mama ulimwenguni. Madini ya thamani yanapatikana ardhini, miti ya mbao inapatikana ardhini pamoja na mimea ya kila aina, bila kusahau kwamba viumbe hai wengine, binadamu na hayawani wa mwituni, nao pia wanaitegemea ardhi kwa ajili ya ustawi wao, kwani udongo huu unatumika kuzalisha kitu chochote ambacho kinahitajika kwa matumizi ya binadamu na wanyama.
Tumeirithi ardhi kutoka kwa vizazi vilivyotangulia ikiwa na ubora wa asili, lakini kutokana na matumizi ya muda mrefu, ardhi hii huzeeka na kushindwa kutoa mazao bora juu yake, hivyo kumfanya binadamu kutafuta namna nyingine ya kuifanya ardhi hiyo itoe mazao bora.
Katika sehemu kubwa ya nchi yetu, ardhi imekuwa chanzo cha migogoro ya mara kwa mara kutokana na matumizi yake, ambapo jamii za wakulima na wafugaji zimekuwa zikigombana – na hata wakati mwingine kusababisha maafa – kila moja ikisema inastahili kutumia ardhi hii.
Hii ni kwa sababu mkulima, baada ya kuona ardhi yake imechoka huamua kutafuta maeneo mengine yaliyo bora na kuanza kuyatumia. Wakati mwingine hulazimika kufyeka misitu ili kupata mashamba mapya, hali ambayo siyo tu inaharibu mazingira, lakini pia inaweza kututia umaskini wa milele kwa sababu ardhi iliyoachwa awali huwa haitafutiwi njia muafaka ya kuifanya irejee kwenye ubora wake.
Katika baadhi ya maeneo, wakulima wengine hutafuta mbolea, hasa za chumvi chumvi, na kuzitumia katika ardhi ile inayoonekana kuzeeka. Lakini matatizo mengi huibuka kutokana na matumizi ya mbolea pamoja na madawa ya kemikali kwenye kilimo. Hii ni kwa sababu mbolea hizi zina kemikali na yale madawa ya kuua wadudu yana madhara yake kwani yana sumu isiyoonekana. Hii sumu tunakula au tunakunywa na ndizo zinazoleta madhara kwa binadamu na udongo.
Aidha, mazao yatokanayo na kilimo cha mbolea hizi za kemikali yanaleta athari kubwa zisizoonekana kwa binadamu na hata wanyama. Lakini jambo la kuzingatia kwa sasa, kila mtu anatakiwa kuvuta kumbukumbu zake kulingana na umri alioishi na kuangalia yafuatayo:
 Hali ya udongo enzi zile na sasa ikoje? 
Kiwango cha maradhi wakati ule na sasa kikoje? 
Uwezo wa udongo kuzalisha mazao umepungua au unazidi mwaka hadi mwaka?
Wengi wetu tumegundua kwamba mbolea za chumvichumvi zimechakaza udongo na hivyo kufanya uzalishaji upungue.
 Hata mazao yatokanayo na matumizi ya mbolea hizo yamekosa ubora wa asili unaotakiwa.
 Hii inatia shaka kama umaskini wa mkulima utakwisha ikiwa hatabadili aina ya pembejeo kuokoa ardhi yake isizidi kuchakaa, na wakati huo huo kupunguza sumu isiyoonekana kwenye udongo na vyanzo vya maji.
Katika mataifa mengi ya ulimwengu wa kwanza, mbolea za chumvi chumvi zinatumika kupandia na kukuzia miti, hasa ya mbao. Vile vile inatumika kutengenezea mazingira kwa maeneo ambayo hayatumiki kuzalisha mazao ya chakula cha binadamu. 
Wao wamekuwa wakipiga sana vita vyakula vilivyolimwa kwa kutumia mbolea za chumvi chumvi, na ndiyo maana hivi sasa katika soko la dunia, bidhaa zilizozalishwa kwa kutumia mbolea hizi za chumvi chumvi zimekuwa zikiuzwa kwa bei ya chini kuliko zile zinazolimwa kwa kutumia kilimo hai. 
Sasa tujiulize, kwa nini sisi tunaendelea kutumia mbolea hizi zinazoua udongo wetu na kuweka sumu?
 Hivi hakuna mbolea nyingine mbadala? 
Jibu ni kwamba, mbolea mbadala zipo.
MBOLEA MBADALA
Mbolea mbadala ni zile zinazotokana na marejea na uozo wa asili. Uozo wa asili unaotokana na majani mbalimbali, samadi ya mifugo asili; mabaki ya nafaka au mazao mbalimbali (kama maganda ya karanga, mabua ya mahindi, n.k.).
Mbolea hizi zinaweza kupatikana au kutengenezwa katika mazao tunayolima, kwenye mazingira tunayoishi. Mbolea hizi zinasaidia kurudisha udongo katika hali ya rutuba na asili yake na gharama za mbolea hizi ni nafuu kabisa na zinadumu ardhini kwa muda mrefu.
ZINGATIA
Jambo la kuzingatia ni kwamba, udongo ni mali pekee yenye thamani kubwa ambayo tumepewa na Mwenyezi Mungu. Hivi sasa kuna migogoro mingi vijijini kutokana na watu kukimbilia mashamba mapya kwa ajili ya kutafuta rutuba baada ya mashamba yao ya zamani kufa kutokana na matumizi ya mbolea zenye kemikali.
Ni ukweli usiopingika kwamba, mbolea za chumvi chumvi zikiisha muda wake hugeuka sumu na baadaye mkulima analazimika kutumia gharama kubwa kuweka mbolea za mboji ili kurudisha udongo katika hali nzuri. Sumu hii isiyoonekana inaharibu udongo, vyanzo vya maji na hata mwili wako mwenyewe.
Mkulima anahitaji kupata mazao bora na ya kutosha ili yamsaidie kwa chakula, na ziada inayopatikana auze kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya familia, lengo ambalo linaonekana kuwa gumu kufikiwa katika nyakati za sasa ambapo pembejeo za kilimo zimekuwa ghali na zaidi matumizi ya mbolea za kemikali yanazidi kuua ardhi, hivyo kupunguza uzalishaji wenyewe.
Aidha, hata mazao yatokanayo na kilimo cha mbolea za kemikali nayo hayana bei kubwa katika soko la dunia ikilinganishwa na mazao yatokanayo na kilimo hai, ambacho kwa sasa ndicho kinachohamasishwa ulimwenguni kwa sababu kinatumia viuatilifu asilia ambavyo siyo tu vinaongeza tija ya mazao, lakini pia ni rafiki wa mazingira.
Kwa mfano, katika mwaka 2003/2004 wastani wa bei za mazao ya kilimo hai ilikuwa takriban asilimia 20 hadi 50 juu ya bei za mazao yasiyo ya kilimo hai katika Soko la Jumuiya ya Ulaya na Marekani. Kwa mwaka 2005/2006 kahawa iliyozalishwa kwa kilimo hai (organic coffee) iliuzwa kwa Dola za Kimarekani (USD) 65.7 kwa kilo 50 ikilinganishwa na USD 50.0 kwa kilo 50 za kahawa iliyozalishwa kwa kutumia kemikali za kilimo (agro-chemicals). Aidha, vanilla iliyouzwa nchi za Jumuiya ya Ulaya ilipata premium ya asilimia 20 hadi 300.
Kilimo hai au organic farming ni aina ya kilimo kinachozingatia matumizi endelevu ya rasilimali za uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo. Kilimo hicho kinatumia mbolea na madawa yasiyotengenezwa viwandani na kinazingatia utunzaji wa mazingira kwa ajili ya manufaa kwa jamii, kiuchumi na kiafya.
Ili bidhaa zikubalike katika Soko la Kimataifa kuwa zimezalishwa kwa kutumia mbinu za kilimo hai, zinapaswa kwanza kupitishwa na Taasisi zinazosimamia ubora wa bidhaa hizo. Taasisi hizo ni International Federation of Organic Agriculture Movement (IFOAM) na Shirika la Ubora wa Viwango vya Vyakula la Umoja wa Mataifa (Codeaux Alimentarius Commission). Soko la mazao ya kilimo hai hutegemea walaji wa mazao hayo ambao wapo tayari kulipa bei kubwa kwa mazao ambayo yamezalishwa bila ya kutumia viatilifu na mbolea za viwandani.
Kilimo hai nchini kilianza kupata umaarufu katika miaka ya 1990 baada ya Serikali kuruhusu Taasisi kadhaa zisizo za Kiserikali (NGO) zikiwemo EGAJ, INADESTZ, PELUM, Meatu Cotton Projects, Babati LAMP na nyinginezo zilizojitokeza kueneza elimu na teknolojia za kilimo hai.
Aidha, Serikali kwa kutambua umuhimu wa kilimo hai na nia ya kuwasaidia wakulima kuendeleza kilimo hicho imeweka vipengele muhimu kwenye sera yake ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuruhusu Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kusimamia biashara na bidhaa zake ambapo mwaka 2005 iliruhusu kuundwa kwa Tanzania Organic Agriculture Movement (TOAM) yenye lengo la kuwaunganisha wadau wa kilimo hai na kuwajengea uwezo.
Kutokana na juhudi hizo hivi sasa kilimo hai kinalimwa katika Mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Kigoma, Iringa, Pwani, Kagera, Mbeya, Morogoro, Shinyanga na Arusha. Mazao yanayozalishwa kwa njia ya mkataba ni pamoja na kahawa, chai, korosho, cocoa na pamba. Mazao mengine ni matunda na viungo hususan mananasi, tangawizi, tumeric, vanilla, pilipili na vitunguu. Sehemu kubwa ya bidhaa wanazozalisha zinauzwa moja kwa moja katika Soko la Jumuiya ya Ulaya na kiasi kidogo katika Soko la Marekani.
Hata hivyo, masharti yanayoambatana na kilimo hai yanakuwa magumu kwa baadhi ya wakulima na hivyo wakulima wengi kushindwa kuzalisha mazao hayo pamoja na kuwa yana bei kubwa.
Utafiti wa kina unafanywa na Mashirika ya Nchi za Afrika Mashariki ambayo ni Kenya Organic Agricultural Network (KOAN), National Organic Agricultural Movement of Uganda (NGAMU) na Tanzania Organic Agricultural Movement (TOAM) ili kuboresha uzalishaji na fursa za biashara ya bidhaa za kilimo hai katika nchi za Afrika Mashariki. Matokeo yatatolewa baada ya utafiti kukamilika.
Kilimo hai ni muhimu sana nchini Tanzania na mkombozi wa mkulima kwa kuwa kitamfanya kudumu mahali pamoja kwa muda mrefu na kuweza kujipanga vyema namna ya kujikwamua kimaisha. Pia kilimo hai kitainusuru nchi isigeuke jangwa kutokana na watu wanaokimbilia kufyeka misitu kwa minajiri ya kutafuta ardhi yenye rutuba, na zaidi kitasaidia kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji ambayo inatokea sasa.
Mikakati ya kuhamaisha kilimo hai ni elimu ya uhamasishaji ambayo inatakiwa ianzie ngazi ya chini, kwa mkulima mmoja mmoja, kwa vikundi tukitumia viongozi wa vijiji, kata, wilaya, mikoa na taifa ili kila mtu afahamu faida zake kwa ukamilifu.
Uwepo wa pembejeo za mboji nchini utamkwe kwa wananchi na serikali yenyewe. Hii itasaidia wakulima waelewe haraka na itasaidia kuharakisha watu wanaotaka kuweka miradi ya kutengeneza pembejeo hizo hapa nchini wapate mwelekeo mzuri.
Pembejeo za mboji pia zinapaswa kutambuliwa na kuingizwa kwenye ruzuku kama pembejeo zingine ili mkulima apate unafuu na serikali haipaswi kupendelea zaidi mbolea za kemikali.
Serikali inatakiwa kuongeza juhudi zaidi katika kuhamasisha wananchi waendeleze kilimo hai, ambacho ni endelevu na rafiki wa mazingira, ili kiwanufaishe zaidi kwani mazao yatokanayo na kilimo hicho yana uhakika wa soko ulimwenguni tofauti nay ale yanayotumia mbolea za kemikali.
Kukaa kimya kwa serikali kunamaanisha kwamba hata wadau wanaojitokeza kushabikia kilimo hai nchini watakata tamaa, kwani hata mbolea asilia wanazoziagiza kutoka nje ama kuzitengeneza zinakosa soko kutokana na wakulima kutokuwa na elimu na maafisa kilimo kugoma kuhamasisha utumiaji wa mbolea hizo kwa maelezo kwamba hawajapewa maagizo kutoka wizarani.
Kama kweli tunataka kujikomboa kupitia kilimo, kwa kweli hatuna budi kutumia zaidi kilimo hai ambacho pia kinaweza kutuepusha na migogoro ya ardhi kama inayojitokeza sasa baina ya wakulima na wafugaj

Monday 6 May 2013

UMUHIMU WA KILIMO CHA MAZAO TOFAUTI

Kila mwananchi anapaswa kujishughulisha na kilimo cha mazao mbalimbali ili aweze kuendesha maisha yake hususani  katika mahitaji ya familia ikiwemo kusomesha pamoja na kujipatia mahitaji mbalimbali katika kuendesha maisha ya kila siku.

Katika kufanikisha hili serikali imekuwa ikitilia mkazo suala la kilimo kwa wananchi waliopo vijijini na Mjini ili kuweza kukabiliana na njaa  katika jamii ambayo imekuwa ikitokea  kwa wananchi hasa waishio vijijini ambao kwa kiasi kikubwa wao ndo wamekuwa wakikubwa na adha hiyo.

Wananchi wamekuwa na jitihada zaa kuhakikisha wanalima na kupata mazao bora ambayo yanaweza kuwazesha kupata masoko ya uhakika kutokana na ubora unaokuwepo katika mazao yao, lakini pia hata suala la pembejeo ambalo ni muhimu kwa mkulima ili aweze kuvuna mazao mengi kutokana na kutumia njia za kisasa.

Hivi karibuni mwandishi wa makala haya alitembelea Mashamba ya Vitunguu  maji yaliyopo katika Kata ya Igomelo wilaya ya Mbarali kuona shughuli zinazofanywa na wakulima hao na  kujishughulisha na kilimo cha vitunguu ambacho nkimekuwa kikilimwa kwa wingi katika Wilaya hiyo.

Kilimo hicho cha vitunguu ambacho kimekuwa kikilimwa kwa njia ya umwagiliaji kimekuwa kikileta  tija kwa wakulima licha ya kuwa vitunguu vimekuwa havina soko na hivyo kubaki kuuza kwa bei ya chini,na hata kwa upande wa  pembejeo imekuwa tatizo kutokana kuuzwa kwa bei  juu na hivyo kuwalazimu wakulima kushindwa kununua pembejeo hizo.

Akizungumza na gazeti hili mmoja wa wakulima wa Skimu ya umwagiliaji ya Igomelo Bw.Daudi Kidange anasema kuwa  katika kilimo hicho wamekuwa wakilima kwa nguvu nyingi lakini tatizo limekuwa ni soko kwao na hivyo kulazimika kuuza kwa bei ya chini licha ya kutumia nguvu nyingi.

Anasema kuwa licha ya kilimo hicho cha umwagiliaji kuwa kizuri lakini bado kuna tatizo la soko la vitunguu kwa wakulima hao.

“Kupitia hiki kilimo cha umwagiliaji mimi nalima Mihogo,Mahindi pamoja na nyanya lakini zao langu kuu ni vitunguu tu ambavyo vimekuwa vikinisaidia kuendesha maisha yangu na familia yangu haya mengine ni ya ziada tu”anasema Mkulima huyo.

Mkulima Mwingine Bw.Gerald Mwalongo anasema kuwa kupitia kilimo cha vitunguu amepata manufaa makubwa kwasababu kwa mwaka analima mara tatu kwa mazao tofauti lakini kitunguu ndo zao pekee ambalo linafanya aendeshe maisha yake.

Anasema kuwa hapo nyuma hawakuwa  na uwezo wa kusomesha  watoto lakini baada ya kuanzqa kilimo cha vitunguu wameona manufaa kutokana na watoto wao kusoma na hata kuendesha maisha yao ambayo awali hayakuwa mazuri na kusema kuwa toka ameanza kilimo hicho ana miaka minne  na mpaka sasa anaendelea na kilimo cha vitunguu.

“Sawa tunalima na mazao mengine lakini tegemeo kubwa hapa ni kilimo cha  vitunguu ambapo  wote tuliopo kwenye hii skimu ya umwagiliaji asilimia kubwa ni kilimo cha vitunguu  ambacho ni tegemeo kubwa kwa sisi wakulima”anasema.

Akizungumzia kuhusu changamoto za kilimo hicho Bw.Mwalongo anasema kuwa pembejeo imekuwa ni tatizo kubwa kwa wakulima  kutokana na bei kupanda kila siku  hivyo kumfanya mkulima wa hali ya chini kushindwa kumudu pembejeo hizo.

Mkulima huyo anasema kuwa   kutokana na pembejeo hizo kuwa bei juu ni vema serikali ikachunguza ushuru ili kuweza kuingiza bila ushuru ili wakulima waweze kununua kwa bei ya chini.

Akiongelea kuhusu Soko la Vitunguu  Bw. Mwalongo anasema hawana soko maalamu la kuuzia vitunguu kwani wakishalima wateja wanakuja shambani moja kwa moja kwa kununua bei yeyote wanayotaka wanunuzi hao,kwa sehemu kubwa wao ndo wapangaji wa bei kwasababu bei ikipangwa na wakulima wenyewe wanakuwa hawaridhiki.

Kufutia kukosa Soko hilo anasema mara nyingi wamekuwa wakiomba serikali iwatafutie soko la vitunguu lakini bado hakuna kinachoendelea.

Hata hivyo anasema kuwa wanunuzi wa vitunguu hivyo wanatokaTunduma,Malawi,CongoRuvuma, kwa upande wa Dar ni mara chache kutokea.

Akizungumzia kuhusu bei  mkulima huyo anasema kwa gunia moja huuzwa kati ya sh.3,0000 mpaka 25,000 hali ambayo inaathiri maisha ya wakulima.

“Tunaomba serikali itusaidie kupata soko kwani kwa bei hii tunayouza ni unyonyaji mkubwa ukijitahidi sana unauza sh.70,000 kwa gunia moja.

Mkulima mwinginwe Bi. Ashiza Mwogofi ambaye ni mkazi wa Igawa anasema kwa upande wa soko mwaka hadi mwaka hadi  vimekuwa havina soko.

Bw.Raphael Bendo anasema  tatizo  kubwa lililopo kwa wakulima ni gharama ya pembejeo na ukosefu wa soko hali hiyo inaathiri wakulima kutokana na wanunuzi kuja kwenye mashamba kwa pamoja hivyo inakuwa ngumu kwa mkulima kuwa na sauti ya pamoja.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Skimu  ya Umwagiliaji ya Igomelo Bw.Luhana Mpinga anasema skimu hiyo ina wanachama 315,wanachama wamekuwa wakijikomboa kupitia kilimo cha umwagiliaji lakini tatizo ni soko la vitunguu.

Tatizo kubwa lililopo ni kutokuwa  na soko la uhakika, maghara ya kutunzia mazao kwani yaliyopo si ya kisasa kuna umuhimu serikali ikawajali wakulima kwa sehemu fulani.

Hata hivyo anasema wafanyabishara wamekuwa wakiwarubuni wakulima kwa kuongeza ujazo kwenye magunia wakati serikali ilishakata mtindo wa LUMBESA.

Naye Ofisa Kilimo na Mifugo Wilaya ya Mbarali Bw. Dickson Maruchuanasema wameanza kujenga miundo mbinu ya masoko ya vitunguu, katika maeneo ya Chimala,Mbuyuni,hata hivyo anasema wamewahamasisha wakulima wajiunge kwenye vikundi.

Aidha Bw. Maruchu anasema mwaka 2013 wanatarajia kujenga  visoko vidogo ambako kutakuwa na mashine za usindikaji  ili viweze kuwasaidia wakulima katika mazao yao wanayolima.

SABABU ZA KASUKU/CHIRIKU KUJIDONOA MANYOYA




1 - Lishe duni, upweke na kukosa matunzo ya jumla

2 - Kama atakuwa anatafuna kucha zako unapomshika

3 - Viroboto au utitiri

4- Maambukizi ya bakteria au fangasi

5 - Banda dogo sana

6 - Lishe yenye vitamini A kwa wingi zaidi

NINI KIFANYIKE
1 - Hakikisha ndege wako anapata mlo kamili, unaweza kununua chakula kwenye maduka au ukachanganya mwenyewe baada ya kupata utaalam, apate matunzo yote muhimu na pia asiwe mwenyewe ni vizuri ukafuga dume na jike.

2 - Kama unatabia ya kumshika ndege wako hakikisha unavaa kitu cha kukinga asiweze kula kucha zako kama vile gloves

3 - Viroboto na uttiiri vidhibitiwe kwa kutumia dawa maalum kama vile akheri powder

4 - Maambukizi ya bakteria na fangasi yadhibitiwe mara moja kwa kutumia dawa kama ancobal

5 - Hakikisha ndege wako anaishi kwenye banda lenye ukubwa wa kutosha

6 - Punguza vyakula vyenye vitamini A kwa wingi kama vile karoti na mapapai